BEKI wa kulia wa timu ya wananchi- Yanga SC. Paul Godfrey Nyang’anya maarufu kama ‘Boxer’ amepata pigo baada ya kuondokewa na baba yake mzazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Jangwani, kifo cha mzazi huyo wa Boxer kimetokea leo jijini Dar es Salaam.
Taarifa hiyo iliyotolewa kwenye akaunti rasmi ya Yanga katika mtandao wa Instagram, imesema; ” Klabu ya Yanga imepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Baba mzazi wa mchezaji wetu, Paul Godfrey Nyang’anya klilichotokea leo jijini Dar es Salaam.
“Kwa niaba ya wanachama, wapenzi na mashabiki wa Yanga, uongozi wa Yanga unatoa pole kwa mchezaji wetu Paul na familia yake yote kwa msiba huo mzito na kwamba klabu iko pamoja naye katika kipindi hiki cha majonzi. Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe.”
Leave a comment