RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo tarehe 02 Julai, 2023 ametengua uteuzi wa wakuu wa wilaya ya Kilindi na Temeke na kuteua wengine wapya. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunusi, katika mabadiliko hayo madogo ya Wakuu wa Wilaya; Rais Samia ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Athumani Munkunda na kumteua Mobhare Holmes Matinyi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.
Pia metengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Abel Yeji Busalama. Amemhamisha kituo Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini, Hashim Shaib Mgandilwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi.
Taarifa hiyo imesema, Rais Samia amemteua James Wilbert Kaji kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini.
Leave a comment