RAIS Samia Suluhu Hassan amemteua Prof Said Shehe Aboud kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Prof. Aboud ni Profesa Mshiriki na Kaimu Mkurugenzi wa Mipango, Fedha na Utawala, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 20 Oktoba, 2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus imesema Prof. Aboud anachukua nafasi ya Prof. Yunus Mgaya amemaliza muda wake mwezi Septemba, 2022.
Leave a comment