RAIS Samia Suluhu Hassan amefanya
uteuzi na utenguzi wa viongozi mbalimbali ikiwamo utenguzi Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Richard Rwanyakaato Kiza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kiza ambaye awali alikuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa uhifadhi kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA),tarehe 12 Oktoba mwaka jana aliteuliwa na Samia kuwa Kamishna wa Uhifadhi Ngorongoro.
Katika taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunusi ni kwamba Rais Samia amemteua Ally Senga Gugu kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Kabla ya uteuzi huu, Gugu alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma.
Pia amemteua Kaspar Kaspar Mmuya kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma. Kabla ya uteuzi huu Mmuya alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Taarifa imeeleza pia kuwa Rais Samia amemteua Mhandisi Mwajuma Waziri kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji. Kabla ya uleuzi huu Mhandisi Waziri alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji.
Mhandisi Waziri anachukua nafasi ya Prof. Jamal Katundu ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Pia amemteua Ephraim Mafuru kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB). Kabla ya uteuzi huu Bw. Mafuru alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Mafuru anachukua nafasi ya Damasi Mfugale ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Asante kwa taarifa