RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania wote kuendelee kudumisha haki, umoja, amani na mshikamano kwenye Sikukuu ya Eid al -Fitr. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kupitia kurasa rasmi za mitandao za mkuu huyo wa nchi leo tarehe 10 Aprili 2024, Rais Samia ameandika; “Nawatakia Watanzania wote kheri ya Sikukuu ya Eid al-Fitr, tukimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa baraka ya kuhitimisha funga na ibada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
“Mwenyezi Mungu atuonaye tunaposimama na mageuko yetu kati ya wanaosujudu, Mwenye kusikia na kupokea dua zetu; aendelee kutubariki na kudumisha Taifa letu katika haki, umoja, amani na mshikamano; katika misingi ya kufanya yaliyo mema, kujali na kutumikia wengine kwa upendo na weledi, na mioyo iliyojaa shukrani na ibada kwake” ameandika Rais Samia.
Nawatakia Watanzania wote kheri ya Sikukuu ya Eid al-Fitr, tukimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa baraka ya kuhitimisha funga na ibada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Mwenyezi Mungu atuonaye tunaposimama na mageuko yetu kati ya wanaosujudu, Mwenye kusikia na kupokea… pic.twitter.com/R3TWFowzia
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) April 10, 2024
Leave a comment