Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia asamehe wafungwa 3,826
Habari Mchanganyiko

Rais Samia asamehe wafungwa 3,826

Spread the love

KATIKA kuadhimisha miaka 58 ya Muungano wa Tanzania leo tarehe 26 Aprili, 2022, Rais Samia Suluhu Hassan amesamehe wafungwa 3,826. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Samia amechukua hatua hiyo kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni wafungwa hao wametokana na masharti 18 ya vifungo vyao.

Masharti hayo ni pamoja na wafungwa wagonjwa wenye magonjwa ya kudumu ambao wametumikia robo ya vifungo vyao na wapo kwenye ‘terminal stage’, ugonjwa huo uthibitishwe na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa na wilaya.

“Wafungwa wazee wenye umri wa miaka 70 au zaidi ambao wametumikia robo ya vifungio vyao. Umri huo uthibitishwe na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa mkoa au wilaya.

“Wafungwa wa kike walioingia gerezani wakiwa na watoto wanaonyonya, wasionyonya na wajawazito ambao wametumikia robo ya vifungo vya.

“Wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili ambao wametumikia robo ya vifungo vyao. Ulemavu huo uthibitishwe na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa mkoa au wilaya,” imesema taarifa hiyo.

Wafungwa wengine ni waliohukumiwa aadhabu ya kuwekwa kizuizini ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka 10 na kuendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yashiriki maadhimisho Mei Mosi Arusha

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeungana na maelfu ya...

Habari Mchanganyiko

Makonda autaka mgodi kubadilisha maisha ya wana-Geita

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametoa wito kwa...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Je, miji ya Uingereza inafilisika?

Spread the loveMNAMO 1890, mwandishi mmoja wa habari Mmarekani aitwaye Julian Ralph...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

error: Content is protected !!