Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Tajiri namba 1 duniani ainunua Twitter
Kimataifa

Tajiri namba 1 duniani ainunua Twitter

Elon Musk
Spread the love

 

MUASISI wa kampuni ya magari ya Tesla, Elon Musk ambaye pia ni tajiri namba moja duniani, amenunua kampuni ya mtandao wa kijamii ya Twitter kwa dola za Kimarekani bilioni 44 (Sh trilioni 102.2). Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 25 Aprili, 2022 na mmoja wa wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni hiyo, Bret Taylor imeeleza kuwa chini ya mkataba huo, wenye hisa watapokea dola 54.20 (Sh. 125,920) kwa kila hisa.

Makubaliano hayo yanatarajiwa kukamilika rasmi mwaka huu. Hii ina maana kuwa mojawapo ya makampuni makubwa kabisa ya mitandao ya kijamii duniani itamilikiwa na mtu mmoja.

twitter

Musk mwenye wafuasi zaidi ya milioni 84 katika mtandao huo, amesema atazingatia zaidi katika kuruhusu uhuru wa kujieleza kwenye jukwaa hilo.

Amesema alitaka kuumiliki mtandao huo wa kijamii na kuufanya kuwa wa kibinafsi kwa sababu anahisi kuwa hautimizi uwezo wake wa kuwa jukwaa la uhuru wa kujieleza.

Awali, kampuni hiyo inayomilikiwa na wanahisa mbalimbali, ilijaribu kulizuia pendekezo la Musk, lakini baada ya mkutano mrefu kati yake na wanahisa hao mwishoni mwa wiki iliyopita, ikaridhia ombi hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!