Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Rais Samia akagua ujenzi wa kituo cha afya Kizimkazi kinachojengwa na Serikali, NBC
AfyaHabari Mchanganyiko

Rais Samia akagua ujenzi wa kituo cha afya Kizimkazi kinachojengwa na Serikali, NBC

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ametembelea ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kizimkazi kilichopo Mkoa wa Kusini Unguja kinachojengwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ikiwa ni jitihada za wadau hao wawili katika kuimarisha huduma za afya kwa wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Ziara ya Rais Samia kwenye eneo hilo la mradi imefanyika leo Alhamisi ikiwa pia ni sehemu ya ufungaji wa Tamasha la Kizimkazi 2023.

Rais Samia Suluhu Hassan (kushoto) akimsikiliza Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Zanzibar, Ramadhan Lesso (wa tatu kushoto) wakati akielezea huduma zinazotolewa na benki hiyo.

Katika ziara hiyo Rais Samia aliambatana na viongozi waandamizi kutoka serikalini na Chama tawala cha CCM  akiwemo Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadidi, viongozi waandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Theobald Sabi pamoja na wakazi wa eneo hilo.

Rais Samia Suluhu Hassan (kushoto) akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Rashid Hadidi (wa pili kulia), Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo (Kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya NBC Theobald Sabi (wa tatu kulia) wakati wa hafla hiyo.

Akizungumzia mradi huo wenye thamani ya Sh 4.4 bilioni ambapo benki ya NBC imechangia kiasi cha Sh 400 milioni, Rais Samia pamoja na kuipongeza NBC kwa hatua hiyo muhimu.

Mafundi wakiendelea na ujenzi wa mradi wa kituo cha Afya cha Kizimkazi kilichopo Mkoa wa Kusini Unguja kinachojengwa na Serikali kwa kushirikiana na benki ya NBC.

Amesema ni lengo la serikali kuboresha huduma ya afya kwa kujenga vituo vya afya kwenye maeneo mbalimbali kulingana na uhitaji mkubwa  wa huduma hiyo katika maeneo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!