Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Kikwete: Demokrasia Afrika inapitia changamoto
Habari za Siasa

Rais Kikwete: Demokrasia Afrika inapitia changamoto

Spread the love

RAIS Mstaafu wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete, amesema demokrasia ya barani Afrika, inapitia changamoto nyingine, ambazo baadhi yake zinasababishwa na taasisi zinazosimamia suala hilo kuwa dhaifu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Dk. Kikwete ametoa kauli hiyo leo tarehe 18 Julai 2023, akitoa masuala yaliyojadiliwa katika mkutano wa viongozi wastaafu Afrika kuhusu hatma ya demokrasia.

“Kumekuwepo na tatizo la demokrasia iliyokuwepo, chaguzi zina mashaka lakini pia katika uchambuzi imeonekana kwamba katika demokrasia ya Afrika ushiriki wa wanawake na vijana hauridhishi. Yako matatizo makubwa ya rushwa katika demokrasia zetu lakini udhaifu wa zile taasisi zinazosimamia demokrasia,” amesema Dk. Kikwete.

Mbali na taasisi zinazosimamia demokrasia kuwa dhaifu, Dk. Kikwete amesema changamoto nyingine inayorudisha nyuma maendeleo ya suala hilo ni rushwa na uroho wa madaraka, ambapo katika kipindi cha miaka nane bara hilo limeshuhudia mapinduzi ya kijeshi 21 katika mataifa tofauti.

“Kuna baadhi ya nchi zinapitia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe kama ilivyo Sudan, hakuna mapinduzi lakini majenerali wawili wameamua kuvuruga nchi yao hata wanachopigania haijulikani. Mkishakuwa na mazingira hayo hata demokrasia haiwezekani,” amesema Dk. Kikwete.

Kufuatia changamoto hizo, Dk. Kikwete amesema viongozi wastaafu walioshiriki mkutano huo wametoa maazimio yao juu ya namna ya kuboresha demokrasia, ambayo yatawasilishwa katika Umoja wa Afrika (AU), kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!