Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Qatar yadaiwa kuwa tishio la usalama
Kimataifa

Qatar yadaiwa kuwa tishio la usalama

Spread the love

MATAIFA manne ya kiarabu, yanayoongoza masharti makali dhidi ya Qatar, yanasema kuwa, hatua ya Doha kukatalia mbali masharti hayo magumu dhidi yake, inaashiria nia yake ya kuendeleza sera ya kuhujumu usalama, katika eneo la mataifa ya Ghuba, anaandika Hamisi Mguta.

Kupitia taarifa ya pamoja, Saudia , Milki za kiarabu Misri na Bahrain, zimeonya kuwa, zitatoa hatua nyingine mpya na ngumu zaidi dhidi ya Qatar.

Mataifa hayo manne yalikatisha uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar mwezi uliopita, yakidai kuwa, taifa hilo linafadhili makundi ya kigaidi duniani, kama vile kundi la Muslim Brotherhood nchini Misri, na linashirikiana na hasimu mkuu wa Saudi- Iran.

Rex Tillerson, Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani, anasafiri hadi Kuwait kujadili namna ya kutanzua mtafaruku huo.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson

Qatar imerudia mara kadhaa kuwa, orodha ya masharti hayo, hayana maana kabisa, mojawepo ikiwa kufunga shirika lake la habari la Al Jazeera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!