Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Qatar yadaiwa kuwa tishio la usalama
Kimataifa

Qatar yadaiwa kuwa tishio la usalama

Spread the love

MATAIFA manne ya kiarabu, yanayoongoza masharti makali dhidi ya Qatar, yanasema kuwa, hatua ya Doha kukatalia mbali masharti hayo magumu dhidi yake, inaashiria nia yake ya kuendeleza sera ya kuhujumu usalama, katika eneo la mataifa ya Ghuba, anaandika Hamisi Mguta.

Kupitia taarifa ya pamoja, Saudia , Milki za kiarabu Misri na Bahrain, zimeonya kuwa, zitatoa hatua nyingine mpya na ngumu zaidi dhidi ya Qatar.

Mataifa hayo manne yalikatisha uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar mwezi uliopita, yakidai kuwa, taifa hilo linafadhili makundi ya kigaidi duniani, kama vile kundi la Muslim Brotherhood nchini Misri, na linashirikiana na hasimu mkuu wa Saudi- Iran.

Rex Tillerson, Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani, anasafiri hadi Kuwait kujadili namna ya kutanzua mtafaruku huo.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson

Qatar imerudia mara kadhaa kuwa, orodha ya masharti hayo, hayana maana kabisa, mojawepo ikiwa kufunga shirika lake la habari la Al Jazeera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!