KESHO kunatarajiwa kuanza kwa sherehe za maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Aga Khan alipochaguliwa kuwa imamu Mkuu wa dhehebu la Shia Ismailia ulimwenguni, tukio ambalo lilitokea tarehe 11 Julai, 1957, anaandika Pendo Omary.
Pia, maadhimisho yataenda sambamba na kutambua shughuli za maendeleo zinazofanywa na Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN).
Maadhimisho hayo yatafanyika kwa siku tatu ambapo Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha sherehe hizo mnamo tarehe 9 Julai, 2017.
Profesa Joe Ligalla, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Aga Khan amesema “katika sherehe hizi, tunataka wananchi watambue kwamba kuna mambo mengi yamefanyika kupitia mtandao wa maendeleo wa Aga Khan.
“Si sherehe za kusherehekea tu mtu kuwa Imamu wa kidini lakini tutambue kuwa ni kiongozi aliyeshiriki katika kubuni miradi ya kimaendeleo hapa Tanzania.”
Aidha, AKDN umefanya kazi kubwa ya kuwainua wananchi wa kiapato cha chini na kutoa huduma katika sekta za afya, elimu, kilimo, bima na utalii.
Leave a comment