Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sherehe za miaka 60 tangu Aga Khan kusimikwa uimamu kuanza kesho
Habari Mchanganyiko

Sherehe za miaka 60 tangu Aga Khan kusimikwa uimamu kuanza kesho

Spread the love

KESHO kunatarajiwa kuanza kwa sherehe za maadhimisho ya miaka 60 tangu  Mtukufu Aga Khan alipochaguliwa kuwa imamu Mkuu wa dhehebu la Shia Ismailia ulimwenguni, tukio ambalo lilitokea tarehe 11 Julai, 1957, anaandika Pendo Omary.

Pia, maadhimisho yataenda sambamba na kutambua shughuli za maendeleo zinazofanywa na Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN).

Maadhimisho hayo yatafanyika kwa siku tatu ambapo Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha sherehe hizo mnamo tarehe 9 Julai, 2017.

Profesa Joe Ligalla, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Aga Khan amesema “katika sherehe hizi, tunataka wananchi watambue kwamba kuna mambo mengi yamefanyika kupitia mtandao wa maendeleo wa Aga Khan.

“Si sherehe za kusherehekea tu mtu kuwa Imamu wa kidini lakini tutambue kuwa ni kiongozi aliyeshiriki katika kubuni miradi ya kimaendeleo hapa Tanzania.”

Aidha, AKDN umefanya kazi kubwa ya kuwainua wananchi wa kiapato cha chini  na kutoa huduma katika sekta za afya, elimu, kilimo, bima na utalii.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!