Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lipumba, Maalim Seif siku zinahesabika
Habari za SiasaTangulizi

Lipumba, Maalim Seif siku zinahesabika

Spread the love

KESI ya Madai Na. 21 ya mwaka 2017 iliyopangwa kusikilizwa leo katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam, mbele ya Jaji Wilfred Dyansobera kuhusu wizi wa Sh. 369 milioni, fedha za ruzuku za Chama cha Wananchi – CUF imeahirishwa mpaka tarehe 10, Julai 2017, anaandika Hamisi Mguta.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Bodi ya wadhamini wa CUF, ambapo  watuhumiwa ni pamoja na Jaji Francis Mutungi, Msajili wa Vyama vya Siasa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa chama hicho anayetambulika na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa huku akiwa amefukuzwa uanachama na CUF.

Katika kesi hiyo jopo la mawakili wa upande wa mashtaka linaongozwa na Juma Nassoro, Daim Halfan na Hashimu Mzirai, upande wa utetezi unawakilishwa na mawakili ni Gabriel Malata ambaye ni Wakili wa Serikali Mkuu na Makubi Kunju, wakili wa upande wa Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!