Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lipumba, Maalim Seif siku zinahesabika
Habari za SiasaTangulizi

Lipumba, Maalim Seif siku zinahesabika

Spread the love

KESI ya Madai Na. 21 ya mwaka 2017 iliyopangwa kusikilizwa leo katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam, mbele ya Jaji Wilfred Dyansobera kuhusu wizi wa Sh. 369 milioni, fedha za ruzuku za Chama cha Wananchi – CUF imeahirishwa mpaka tarehe 10, Julai 2017, anaandika Hamisi Mguta.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Bodi ya wadhamini wa CUF, ambapo  watuhumiwa ni pamoja na Jaji Francis Mutungi, Msajili wa Vyama vya Siasa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa chama hicho anayetambulika na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa huku akiwa amefukuzwa uanachama na CUF.

Katika kesi hiyo jopo la mawakili wa upande wa mashtaka linaongozwa na Juma Nassoro, Daim Halfan na Hashimu Mzirai, upande wa utetezi unawakilishwa na mawakili ni Gabriel Malata ambaye ni Wakili wa Serikali Mkuu na Makubi Kunju, wakili wa upande wa Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!