JESHI la Polisi nchini, limewataka wananchi wapuuze madai ya mauaji ya watu wilayani Kibiti Mkoa wa Pwani, kuibuka tena, likisema hali ni shwari. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Taraifa hiyo imetolewa leo na Jeshi la Polisi kuoitia ukurasa wake wa Twitter, baada ya madai hayo kuibuka hivi karibuni Katika Mitandao ya kijamii.
“Jeshi Polisi limekanusha ujumbe unaosambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na kusema hakuna matukio kama hayo, Kibiti ni shwari na salama. Upuuzeni uzushi huu, pia endeleeni kuwapuuza wasioitakia mema nchi yetu,” imesema taarifa yetu.
Miaka kadhaa iliyopita mauaji ya baadhi ya raia, viongozi wa Serikali za mitaa na Polisi yaliibuka katika wilaya za Mkoa wa Pwani, ikiwemo Kibiti.
Vyombo vya ulinzi na usalama, vilifanikiwa kudhibiti mauaji hayo.
Leave a comment