BALOZI na Mwanasiasa maarufu nchini, Dk. Wilbroad Slaa anadaiwa kukamatwa na Jeshi la Polisi nyumbani kwake Mbweni jijiji Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).
Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali, akiwamo Askofu Emmaus Mwamakula zinasema, Dk. Slaa amekatwa leo Jumapili mchana ikiwa ni siku moja baada ya kukamatwa kwa Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyagali.
Dk. Slaa ambaye pia aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, ni mmoja wa wanasiasa wanaopinga mkataba wa uwekezaji kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai.
Kukamatwa kwa Dk. Slaa pamoja Mwabukusi kumekuja siku chache baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi kuutangazia ulimwengu, kwamba “kuna njama za kumuangusha Rais wa Jamhuri, Dk. Samia Suluhu Hassan.”
Akiandika kupitia mtandao wake wa kijamii, Askofu Mwamakula anasema,
“taarifa zilizotufikia hivi punde ni kuwa Balozi Dk . Wilbroad Slaa amekamatwa na Jeshi la Polisi nyumbani kwako jijini Dar es Salaam.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online kwa taarifa zaidi.
Leave a comment