Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi waanza uchunguzi tukio la Olesendeka kushambuliwa
Habari za SiasaTangulizi

Polisi waanza uchunguzi tukio la Olesendeka kushambuliwa

Spread the love

JESHI la Polisi nchini, limesema limeanza uchunguzi wa tukio la gari la Mbunge wa Simanjiro (CCM), Christopher Ole Sendeka, kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana, akiwa safarini kuelekea Arusha, akitokea jijini Dodoma. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa ya uchunguzi huo imetolewa leo tarehe 30 Juni 2024 na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, DCP David misime.

“Jeshi la Polisi limepokea taarifa ya mbunge wa Simanjiro na dereva wake wakiwa safarini, gari walilokuwa wanatumia kushambuliwa kwa risasi katika kijiji cha Ngaboko wilayani Kiteto na kwa bahati nzuri hakuna aliyepata madhara,” imesema taarifa ya Kamanda Misime na kuongeza:

“Polisi wanafuatilia tukio hilo kwa karibu sana kwani uchunguzi ulishaanza mara baada ya kupokea taarifa, timu ya wataalamu wa uchunguzi wa matukio yaliyohusisha matumizi ya risasi kutoka makao makuu imetumwa kwenda kushirikiana na timu ya mkoa wa Manyara kuchunguza tukio hilo ili kubaini waliohusika ni akina nani na madhumuni au kusudio lao lilikuwa ni nini.”

Tukio hilo linadaiwa kutokea jana wakati Ole Sendeka anarudi jimboni kwake kupitia njia ya Kiteto, ambapo gari aina ya Double Cabin Silver iliwafuatilia na baadae kuanza kuwafyatulia risasi kadhaa zilizoishia katika gari na kushindwa kuwaathiri waliokuwamo ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!