GARI la mbunge wa Simanjiro (CCM) mkoani Manyara, Christopher Ole Sendeka, limeshambuliwa kwa risasi eneo la Ndaleta, wilayani Kiteto wakati akiwa na dereva wake akielekea jimboni kwake Simanjiro. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Lucas Mwakatundu amesema tukio hilo limetokea jioni ya leo Ijumaa tarehe 29 Machi 2024.
Amesema limetokea eneo la Ndaleta, Wilayani Kiteto wakati Ole Sendeka akiwa na dereva wake akielekea jimboni kwake Simanjiro.
“Ole Sendeka akiwa na dereva wake, gari lao lilishambuliwa kwa risasi ila hawakudhurika ni wazima kabisa,” amesema Kaimu Kamanda Mwakatundu huku akibainisha kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi na hakuna anayeshikiliwa kutokana na tukio hilo.
Kaimu Kamanda amesema kwa sasa Ole Sendeka na dereva wake wapo Kituo cha Polisi Kiteto wakiendelea kuhojiwa kuhusu tukio hilo
Pole sana