Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Pazia kampeni za urais DRC lafunguliwa rasmi
Kimataifa

Pazia kampeni za urais DRC lafunguliwa rasmi

Spread the love

JUMLA ya wagombea urais 26 wanatarajiwa kuanza kampeni leo Jumatatu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambazo zinatarajiwa kudumu kwa mwezi mmoja na kuhusisha pia wagombea wa nafasi ya ubunge.

Takriban wapiga kura milioni 44 waliojiandikisha, kati ya wakazi karibu milioni 100, watamchagua rais  tarehe 20 Desemba 2023. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Pia watawachagua kati ya maelfu ya wagombea ubunge na wajumbe wa serikali za mitaa katika nchi hiyo yenye rasilimali nyingi lakini ikiwa imegubikwa na migogoro na ufisadi.

Kampeni ya mapema imekuwa ikiendelea kwa muda, huku Rais Felix Tshisekedi, ambaye anawania muhula wa pili, akihudhuria hafla nyingi za umma akiwa sambamba na washirika wake wanaosifia utendaji katika uongozi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!