Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Odinga, Ruto wakabana koo uchaguzi mkuu Kenya
Kimataifa

Odinga, Ruto wakabana koo uchaguzi mkuu Kenya

Raila Odinga
Spread the love

 

VINARA wa kinyang’anyiro cha Uchaguzi Mkuu nchini Kenya, Raila Odinga wa Azimio na Dk. Wiliam Ruto wa Kenya Kwanza kimezidi kushika kasi baada ya kura mpya za maoni za Shirika la utafiti la Tifa lenye makao yake jijini Nairobi, kuonyesha kuwa wawili hao wako sawa ki-takwimu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Odinga ambaye ni kiongozi wa upinzani anayewania nafasi hiyo kwa mara ya tano anaongoza kwa asilimia 46.7 na mpinzani wake Ruto ambaye ni naibu rais wa sasa ana asilimia 44.4 ya kura.

Kwa mujibu wa Katiba ya Kenya ili kushinda katika duru ya kwanza kwenye uchaguzi mkuu, mgombea anahitaji zaidi ya nusu ya kura zote angalau asilimia 25 ya kura zilizopigwa katika majimbo takriban nusu miongoni mwa yote 47.

Dk. Wiliam Ruto

Ikilinganishwa na kura za maoni za awali za utafiti wa Tifa, sasa zinaonyesha kuwa kura za Ruto zimepungua dhidi ya Odinga ambaye awali alikuwa na asilimia 42 dhidi ya asilimia 39 za Ruto.

Kura za maoni zinaonyesha kuwa Odinga ana uungwaji mkono zaidi katika maeneo ya Nyanza, magharibi ya Kusini ya Rift, Nairobi na sehemu za Lower Eastern, wakati Ruto ana uungwaji mkono zaidi katika maeneo ya kati ya Rift na Mlima Kenya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!