Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kiboko ‘babu’ aliyeua watu 8, auawa
Habari Mchanganyiko

Kiboko ‘babu’ aliyeua watu 8, auawa

Spread the love

KIBOKO dume ambaye kwa muda mrefu amekuwa akisumbua wananchi wa kata ya Mabilioni wilayani Same Mkoa wa Kilimanjaro na kukwamisha shughuli za maendeleo kama kilimo, ufugaji na uchotaji wa maji katika Mto Pangani, ameuawa kwa kupigwa risasi katika msako ulioongozwa na vikosi kutoka TAWA. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkuu wa Wilaya ya Same, Edward Mpogoro akizungumza baada ya kiboko Babu kuuawa.

Kiboko huyo aliyepewa jina la Babu ambaye ameua watu zaidi ya sita, ng’ombe 8, punda na mbuzi tangu mwaka 2017 alikuwa akihusishwa na imani za kishirikina kwani jitihada mbalimbali za kumdhibiti hazikufanikiwa katika kipindi chote

Tarehe 17 Juni 2022 kiboko huyo alimuua kwa kumshambulia mwanaume mmoja aliyekuwa anakwenda shambani kumwagilia ndipo Mkuu wa Wilaya ya Same, Edward Mpogolo alipoagiza kuhakikisha kila mbinu zinatumika kumuua kiboko huyo ili wananchi warudi kufanya shughuli za maendeleo kwa amani.

Baada ya kuanza msako kiboko huyo aliuawa tarehe 28 Julai 2022 saa 11 alfajiri baada ya kuweka mtego na kupigwa risasi ya kichwa na Mzee Ally Miraji Sengela (hunter) aliyesaidiwa na Mzee Fue Omary Ngerwa (Mvuvi na Mweka Mtego) kwa kushirikiana na wahifadhi wa TAWA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

Habari Mchanganyiko

Dereva ajali iliyoua wanafunzi Arusha afikishwa kortini, aomba apelekwe rumande

Spread the loveDEREVA aliyehusika katika ajali la basi la Shule ya Msingi...

error: Content is protected !!