Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo NMB yadhamini milioni 25 michuano ya Golf- Lugalo
Michezo

NMB yadhamini milioni 25 michuano ya Golf- Lugalo

Spread the love

BENKI ya NMB imetoa udhamini wa Sh. milioni 25 kwa Mashindano ya Gofu ya Mkuu wa Majeshi Tanzania (NMB CDF Trophy 2022), kama muendelezo wa sherehe za kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambayo hufanyika Septemba mosi.

Sherehe za kumbukumbu hizo kwa mwaka huu yamelazimika kusogezwa kwa mwezi mmoja kutokana na sababu mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza wakati akipokea mfano wa hundi Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo, ameishukuru  Benki ya NMB kwa kuwa mdhamini wa muda mrefu na kufanyia maboresho zaidi kwa mwaka huu.

Alisema timu mbalimbali zimethibitisha kushiriki michuano hiyo, ambayo itahusisha makundi ya Watoto (junior), Madaraja (division) ya A, B, na C, pamoja na wanawake na Seniors.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Wateja Maalum wa Benki ya NMB, Getrude Mallya, alisema benki yake imedhamini mashindano hayo kwa Sh. milioni 25.

Pia aliwaalika viongozi wa  klabu ya gofu Lugalo kushiriki mbio za NMB Marathon 2022  ‘Mwendo wa Upendo’ zitakazofanyika Oktoba 1, 2022 katika viwanja vya Leaders Club kwa lengo la kukusanya Sh. milioni 600 za kusaidia matibabu ya kina mama wenye matatizo ya fistula nchini.

Mashindano ya Gofu yatafanyika Oktoba 1 hadi 2 mwaka huu kwenye Viwanja vya Gofu Lugalo, jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!