Benki ya NMB imeibuka mshindi wa jumla kitaifa katila kundi la mlipa kodi mkubwazZaidi Tanzania lakini pia katika kundi la mlipa kodi bora zaidi anayelipa kodi kwa hiari. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
NMB imenyakua tuzo hizo jana Ijumaa katika hafla ya walipa kodi wakubwa kwa 2022/2023 iliyofanyika jijini Dar es salaam.
Ushindi huo unaifanya NMB kubeba tuzo hizo zinazotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa mwaka wa pili mfululizo
Jumla ya tuzo ilizopata NMB ni: Mshindi wa jumla kitaifa: Taasisi inayolipa Kodi kubwa zaidi nchini Tanzania (Sekta zote).
Pili, Mshindi wa jumla kitaifa: Taasisi bora inayolipa kodi kwa hiari kwa kuzingatia misingi na kanuni bora za ulipaji kodi (Most Compliant Tax Payer).
Tatu ni mshindi wa kwanza: Mlipa kodi mkubwa zaidi katika kundi la taasisi za fedha nchini Tanzania (mara ya tatu mfululizo).
Akizungumza baada ya kupokea tuzo hizo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna alisema tuzo hizo ni matokeo chanya ya misingi imara ya utawala bora na uadilifu, kuzingatia kanuni za ulipaji kodi, ufanisi katika kuendesha biashara na ubunifu wa suluhishi bora za kifedha kwa wateja.
Ruth Zaipuna aliwashukuru wateja wa NMB na Watanzania wote kwa kuendelea kuiamini benki hiyo kama mshirika wao kwenye biashara na shughuli zao.
“Ninaishukuru Serikali kwa kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya kufanya biashara nchini na kipekee nawashukuru wafanyakazi wenzangu wote wa NMB kwa kuendelea kufanya kazi kwa ari, bidii na kwa uzalendo mkubwa kwa maslahi mapana ya Benki na nchi yetu kwa ujumla,” alisema.
Tuzo hizo za TRA zimetolewa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Dotto Biteko katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
“Kama mdau wa maendeleo, NMB tutaendelea kuendesha biashara yetu kwa kuzingatia sheria na kanuni za nchi ili kuendelea kuchangia kikamilifu ujenzi wa uchumi wa Taifa letu,” alisema Zaipuna.
Leave a comment