Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amtumbua Naibu Waziri – Pauline Gekul
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia amtumbua Naibu Waziri – Pauline Gekul

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumamosi ametengua uteuzi wa Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria, Pauline Philipo Gekul. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Zuhura Yunus haikueleza zaidi sababu za kutenguliwa kwa Mbunge huyo wa Babati Mjini kupitia CCM.

Kabla ya kutenguliwa kwake, kuanzia jana kumeibuka taarifa katika mitandao ya kijamii zikidai mbunge huyo kuwa anatuhumiwa kumtendea ukatili mfanyakazi wake kijana aliyekuwa anamtuhumu kutaka kumuwekea sumu huko Babati mkoani Manyara.

Ikumbukwe kuwa Gekul ambaye awali alikuwa kada wa Chadema, alipata ubunge mwaka 2015 kupitia chama hicho kabla ya mwaka 2021 kuhamia CCM kisha kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Habari, utamaduni, sanaa na michezo kabla wizara hiyo haijagawanywa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!