Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumamosi ametengua uteuzi wa Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria, Pauline Philipo Gekul. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Zuhura Yunus haikueleza zaidi sababu za kutenguliwa kwa Mbunge huyo wa Babati Mjini kupitia CCM.
Kabla ya kutenguliwa kwake, kuanzia jana kumeibuka taarifa katika mitandao ya kijamii zikidai mbunge huyo kuwa anatuhumiwa kumtendea ukatili mfanyakazi wake kijana aliyekuwa anamtuhumu kutaka kumuwekea sumu huko Babati mkoani Manyara.
Ikumbukwe kuwa Gekul ambaye awali alikuwa kada wa Chadema, alipata ubunge mwaka 2015 kupitia chama hicho kabla ya mwaka 2021 kuhamia CCM kisha kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Habari, utamaduni, sanaa na michezo kabla wizara hiyo haijagawanywa.
Leave a comment