Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Majaliwa: Majina wezi wa mapato Mbozi ninayo…
Habari za Siasa

Majaliwa: Majina wezi wa mapato Mbozi ninayo…

Spread the love

Waziri Mkuu Kasim Majaliwa amesema fedha nyingi za mapato yanayokusanywa katika halmashauri kongwe ya wilaya ya Mbozi  mkoani Songwe zinaishia katika mifuko ya watu binafsi ambao majina yao anayo.

Amesema inashangaza halmashauri ya Mbozi inakusanya Sh bilioni nne ilihali Tunduma ambayo ni halmashauri change ikikusanya Sh bilioni 13. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika leo Jumamosi katika stendi ya Malori mkoani hapa, Majaliwa amesema mbali na kukusanya mapato kidogo pia viongozi wa halmashauri hiyo hawana ubunifu wa kubuni vyanzo vipya vya mapato.


Amesema hata hiyo Sh bilioni nne wanayokusanya haionekani inafanya kazi gani kwani miradi yote inajengwa kwa fedha za serikali kuu.

“Mapato ya Sh bilioni nne mnayokusanya kwa mwaka ni kiduchu ukilinganisha na ukongwe wa wilaya, fedha nyingi zinaingia mifukoni mwa watu, majina yote ya wezi ninayo,” amesema.

Awali, mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM) alimuomba waziri mkuu kuipandisha hadhi halmashauri ya Mbozi kuwa manispaa.

Pia amemuomba kutatua changamoto ya ukosefu wa stendi kuu na soko la pamoja la kuuzia mazao.

Akijibu maombi hayo, Majaliwa amesema suala la kupanda hadhi kuwa manispaa sio shida bali tatizo ni vigezo ikiwamo makusanyo ya fedha na mpangilio wa majengo.

“Makusanyo ya Sh bilioni 4 mnazokusanya kwa mwaka ni madogo ukilinganisha na ukongwe wa halmashauri yenu. Tunduma ni wachanga lakini wanakusanya Sh bilioni 13. watumishi, madiwani hamna ubunifu,” amesema Majaliwa.

Amesema Mbozi ni halmashauri kongwe nchini na ina vyanzo vingi vya mapato, ikiwemo makusanyo makubwa yatokanayo na zao la kahawa lakini makusanyo yake ni madogo huku mji huo ukiwa umezorota.

Amesema Tunduma imezidiwa na uwingi wa malori  hivyo halmashauri hiyo inatakiwa kutenga eneo pembezoni mwa barabara na kuweka uzio kwa ajili ya kulaza magari yatakayotozwa fedha na kuingiza kipato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!