KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO, Jens Stoltenberg amesema Urusi imepanga kufanya mashambulizi dhidi ya Ukraine. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Akizungumza katika kongamano la usalama mjini Munich nchini Ujerumani, Stoltenberg, ameliambia shirika moja la utangazaji la Ujerumani kwamba hatari ya shambulio iko juu.
Mashariki mwa Ukraine, mapigano mapya yamezuka katika muda wa wiki moja iliyopita kati ya serikali ya Ukraine na vikosi vinavyotaka kujitenga vinavyoungwa mkono na Urusi.
Takriban visa 2,000 vya ukiukaji wa mapatano ya kusitisha mapigano vilirekodiwa na waangalizi wa Ulaya katika eneo hilo siku ya Jumamosi.
Washirika wa Magharibi wa Ukraine wana wasiwasi kwamba Urusi imejiweka tayari kufanya mashambulio ya kijeshi dhidi ya Ukraine.
Hata hivyo Urusi imekanusha mipango yoyote ya kushambulia taifa hilo jirani.
Wanajeshi wawili wa Ukraine wameuawa na wanne kujeruhiwa kwa makombora siku ya Jumamosi ikiwa ni vifo vya kwanza kuripotiwa katika wiki kadhaa.
Leave a comment