Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa NATO yaonya Urusi kushambulia Ukraine
Kimataifa

NATO yaonya Urusi kushambulia Ukraine

Spread the love

KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO, Jens Stoltenberg amesema Urusi imepanga kufanya mashambulizi dhidi ya Ukraine. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika kongamano la usalama mjini Munich nchini Ujerumani, Stoltenberg, ameliambia shirika moja la utangazaji la Ujerumani kwamba hatari ya shambulio iko juu.

Mashariki mwa Ukraine, mapigano mapya yamezuka katika muda wa wiki moja iliyopita kati ya serikali ya Ukraine na vikosi vinavyotaka kujitenga vinavyoungwa mkono na Urusi.

Takriban visa 2,000 vya ukiukaji wa mapatano ya kusitisha mapigano vilirekodiwa na waangalizi wa Ulaya katika eneo hilo siku ya Jumamosi.

Washirika wa Magharibi wa Ukraine wana wasiwasi kwamba Urusi imejiweka tayari kufanya mashambulio ya kijeshi dhidi ya Ukraine.

Hata hivyo Urusi imekanusha mipango yoyote ya kushambulia taifa hilo jirani.

Wanajeshi wawili wa Ukraine wameuawa na wanne kujeruhiwa kwa makombora siku ya Jumamosi ikiwa ni vifo vya kwanza kuripotiwa katika wiki kadhaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!