Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Musoma Vijiji kumuenzi bingwa wa Kiswahili, Prof. Massamba
Elimu

Musoma Vijiji kumuenzi bingwa wa Kiswahili, Prof. Massamba

Spread the love

WANANCHI wa Musoma Vijijini, mkoani Mara, wameahidi kujenga shule ya sekondari itakayopewa jina la Prof. David Masamba, ili kuuenzi mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili kupitia machapisho mbalimbali aliyoyaandika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara…(endelea).

Ahadi hiyo imetolewa jana tarehe 31 Agosti 2023 na wananchi hao, katika mazishi ya Prof. Massamba, yaliyofanyika  kijijini kwao Kurwaki, mkoani Mara.

Prof. Sospeter Muhongo

Akizungumza katika ibada ya mazishi ya Prof. Massamba, Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, alisema wananchi wamekubali kujenga shule hiyo kijijini Kurwaki, ambako alizaliwa nguli huyo wa Kiswahili, katika eneo la Fonolojia ya Kibantu.

Prof. Muhongo alisema ujenzi wa sekondari hiyo utaanza Septemba 2023.

“Hapa tusitegemee kwanza fedha ya Serikali, tuanze tukijua Serikali inaweza ikatupatia au isitupatie lakini tuanze. Kwa hiyo hili jambo ni jipya sijawahi kusikia Kurwaki wanajitolea, kumbe wanamheshimu sana Massamba,” alisema Prof. Muhongo na kuongeza:

“Kwa kazi alizofanya huyu, vitabu alivyoandika huyu kikao chetu kinaazimia na kinapitisha jina la sekondari litakuwa Prof. Massamba. Hivyo tunajenga sekondari kwa heshima ya ndugu yetu sababu kazi alizofanya hatuwezi tukamzika akapotea hivi hivi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Viwanda zaidi ya 200 kuonyesha bidhaa maonyesho ya TIMEXPO Dar

Spread the loveSHIRIKISHO la Wenye Viwanda Nchini (CTI) kwa kushirikiana na Mamlaka...

Elimu

Wazazi wa wanafunzi waliokosa nafasi vyuo vikuu waonyeshwa njia na GEL

Spread the loveWAKALA wa Elimu ya Vyuo Vikuu Nje ya Nchi, Global Education...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Elimu

Green Acres kuwakatia bima wanafunzi wote

Spread the loveShule ya Green Acres imejipanga kufanya mambo makubwa kwa mwaka...

error: Content is protected !!