Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Musoma Vijiji kumuenzi bingwa wa Kiswahili, Prof. Massamba
Elimu

Musoma Vijiji kumuenzi bingwa wa Kiswahili, Prof. Massamba

Spread the love

WANANCHI wa Musoma Vijijini, mkoani Mara, wameahidi kujenga shule ya sekondari itakayopewa jina la Prof. David Masamba, ili kuuenzi mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili kupitia machapisho mbalimbali aliyoyaandika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara…(endelea).

Ahadi hiyo imetolewa jana tarehe 31 Agosti 2023 na wananchi hao, katika mazishi ya Prof. Massamba, yaliyofanyika  kijijini kwao Kurwaki, mkoani Mara.

Prof. Sospeter Muhongo

Akizungumza katika ibada ya mazishi ya Prof. Massamba, Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, alisema wananchi wamekubali kujenga shule hiyo kijijini Kurwaki, ambako alizaliwa nguli huyo wa Kiswahili, katika eneo la Fonolojia ya Kibantu.

Prof. Muhongo alisema ujenzi wa sekondari hiyo utaanza Septemba 2023.

“Hapa tusitegemee kwanza fedha ya Serikali, tuanze tukijua Serikali inaweza ikatupatia au isitupatie lakini tuanze. Kwa hiyo hili jambo ni jipya sijawahi kusikia Kurwaki wanajitolea, kumbe wanamheshimu sana Massamba,” alisema Prof. Muhongo na kuongeza:

“Kwa kazi alizofanya huyu, vitabu alivyoandika huyu kikao chetu kinaazimia na kinapitisha jina la sekondari litakuwa Prof. Massamba. Hivyo tunajenga sekondari kwa heshima ya ndugu yetu sababu kazi alizofanya hatuwezi tukamzika akapotea hivi hivi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!