Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Museveni akemea mapinduzi Burkina Faso
Kimataifa

Museveni akemea mapinduzi Burkina Faso

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni
Spread the love

 

RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni ameshutumu vikali mapinduzi yaliyotekelezwa nchini Burkina Faso dhidi ya serikali ya Rais wan chi hiyo, Roch Marc Christian Kabore. Anaripoti Mwandishi … (endelea).

Rais Museveni ametoa kauli hiyo jana tarehe 26 Januari, 2022 jijini Kampala nchini Uganda katika hafla ya kuadhimisha miaka 36 tangu atwae hatamu za uongozi nchini Uganda.

Amesema nchi za Afrika ya Magharibi zinatakiwa kujifunza kutoka kwake kuhusu namna ya kuzima wanaopanga mapinduzi.

“Baadhi ya viongozi wengi wa kiraia wanashindwa kuunda jeshi thabiti hivyo wanakuwa katika hatari ya kupinduliwa.

“Ndani ya miaka 10 iliyopita, takribani nchi 10 zimepinduliwa katika eneo la Afrika ya Magharibi. Hatufai kuruhusu hili kufanyika. Hao wanajeshi wanapofanya mapinduzi hawaulizwi chochote na raia kwa sababu hawakuchaguliwa,” amesema.

Amesema vuguvugu la mapinduzi katika nchi za Afrika Magharibi lilianza baada ya Serikali ya Muammar Gaddafi nchini Libya kuangushwa kisha kuzalisha magaidi wengi.

Amesema makundi hayo ya kigaidi yamesambaa katika nchi za Mali, Niger, Guinea, Burkina Faso na nchi nyingine za Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!