WAGONJWA milioni 10.7 wamepona ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) duniani. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kwa mujibu wa mtandao wa worldometer, unaonyesha hadi leo Alhamisi 30 Julai 2020 unaonyesha, walioambukizwa ni milioni 17.1 na waliofariki ni 670,322.
Marekani inaongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi wa COVID-19 ikiwa na maambukiozo milioni 4.5, waliopona milioni 2.2 na waliofariki ni 153,845.
Brazil inafuatia ikiwa na maambukizo milioni 2.5, waliopona milioni 1.51.7 na wagonjwa waliofariki ni 90,188.
China ambako corona ilianzia mwishoni mwa mwaka 2019, ina maambukizo 84,165 ambapo vifo ni 4,634 na waliopona 78,957.
Leave a comment