Jeshi la Polisi mkoa wa Songwe linamshikilia mtumishi mmoja aitwaye Rioba Nyamos (34) ambaye ni Mganga mfawidhi wa Zahanati ya Kijiji Cha Iporoto akiwa anaiba dawa mbalimbali za binadamu mali ya Serikali. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari jana tarehe 21 Julai 2023, Kaimu Kamanda wa mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi wa Polisi Rashid Ngonyani amesema mbinu aliyotumia ni kuficha katika mifuko ya salfeti Ili dawa hizo zisionekane kisha aende kuziuza maeneo ya Mlowo.
Kaimu Kamanda amebainisha dawa hizo kuwa ni Ciprofloxacin box 10, belo 3 za vyandarua, Gauzen absorbent 2 PCs, Vidonge vya uzazi wa mpango Boxi 7, Gauze bunda 02 Surgical gloves boxi 10.
Kutokana na tukio hilo, Kamanda huyo ametoa wito wananchi kutojihusisha na uhalifu kwani Jeshi la Polisi halitosita kuchukua hatua kali dhidi yao.
Pia limewataka watumishi wa Serikali kuacha tamaa kwani Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kwa ajili ya kununua vifaa mbalimbali pamoja na dawa kwa kwa ajili ya kuhudumia wananchi.
Leave a comment