Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia: Serikali iache kiburi, irudi kwenye meza ya mazungumzo
Habari za SiasaTangulizi

Mbatia: Serikali iache kiburi, irudi kwenye meza ya mazungumzo

James Mbatia
Spread the love

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia leo Jumapili ametoa wito kwa Serikali kuacha kiburi na kukubali kurudi kwenye meza ya mazungumzo ili kutafuta suluhu kuhusu mkanganyiko uliojitokeza katika mkataba unaohusu uwekezaji kwenye bandari ya Dar es salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mbatia ametoa wito huo leo tarehe 23 Julai 2023 jijini Dar es Salaam katika mkutano ulioandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Balozi Dk. Willbroad Slaa na wenzie kwa lengo la kujadili kasoro zilizomo katika mkataba wa ushirikiano wa kiserikali kati ya Tanzania na Dubai, kuhusu uwekezaji wa bandari,

Amesema huu ni wakati wa sayansi na teknolojia hivyo ni vema ikubali kukaa na watalaam ili kutoka kwenye mtanzuko huo kwani Taifa likiangamia na wote  wataangamia.

“Ikikubali kukaa kwenye meza ya mazungumzo hakuna kilicho siri, kwenye ulimwengu wa leo hakuna kilicho siri penda tusipende ukweli umewekwa wazi. Turudi pamoja kwenye ubora wa Taifa letu ili libaki kuwa salama… ukiona uovu unatendeka zuia, ukishindwa kuzuia kemea, ukishindwa onesha chuki,” amesema.

Mbatia amesema Taifa lipo katika janga, limegawanyika, linazama hivyo inahitaji hekima ya Mungu ili kurudisha Taifa pamoja.

“Tiba zipo za aina mbili… tutumie ibara ya nane ya katiba ambayo ni nguvu ya umma pili ni watu wenye dhamana kukaa pamoja ili kupata suluhu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!