Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtutura: Wabunge wa CCM wameonewa
Habari za Siasa

Mtutura: Wabunge wa CCM wameonewa

Spread the love

KATIBU wa chama cha ACT-Wazalendo mkoa wa kichama Selou, Abdallah Mtutura amesema kitendo cha CCM kupeleka wabunge wasioweza kuwasema wananchi wao ni kuwaonea wabunge hao. Anaripoti Faki Sosi, Tunduru … (endelea).

“Mtu ukimpa kitu asichoweza kukimudu au kukidhibithi unakuwa umemuonea.”

Kauli hiyo ameitoa leo kwenye ziara ya Katibu Mkuu wa Chama hicho Ado Shaibu kwenye jimbo la Tunduru Kaskazini kata ya Ligula.

Mtutura amesema kuwa asilimia 70 wabunge wa Chama Cha Mapinduzi hawana uwezo wa kuwasemea wananchi bungeni.

Amesema kuwa uchaguzi wa mwaka 2020 haukuwa huru wala wa haki na matokeo yake wakapelekwa watu ambao hawakustahili kuwa wabunge ndio sababu ya kushindwa kuwatetea wananchi bungeni.

Amesema kuwa wabunge hawasemi kama wananchi wanaonewa, tembo wanavamia makazi na mashamba ya watu, hawasemi mgogoro wa wakulima na wafugaji unaoweza kusababisha machafuko.

Mtutura ameongeza kuwa wananchi wamezidiwa na shida hakuna wa kuwasemea. Ametoa wito kwa wananchi kukichagua Chama cha ACT ili wapate sauti mbadala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!