Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa atoa wito NGO’s kufungua akaunti NMB
Habari Mchanganyiko

Majaliwa atoa wito NGO’s kufungua akaunti NMB

Spread the love

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) kufungua akaunti zao katika benki zilizopo nchini kama vile NMB ili kukuza mzunguko wa fedha na uzalendo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Majaliwa jana jijini ametoa wito huo jana tarehe 6 Oktoba jijini Dodoma wakati akizungumza na wananchi na watumishi wa Benki ya NMB alipotembelea banda la benki hiyo katika kilele cha Jukwaa la Mwaka la mashirika yasiyo ya kiserikali.

 

Meneja Mwandamizi Mahusiano Benki ya NMB, Dorah Monyo (kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu, Kassim majaliwa (kulia) alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Jukwaa la mwaka la Mashirika yasiyo ya Kiserikali – Dodoma.

Alisema iwapo mashirika hayi yatafungua akaunti ndani ya benki ya NMB ambayo ina matawi 228 nchi nzima, mbali na kuonyesha uzalendo, lakini itasaidia kuongeza mzunguko wa fedha ndani ya nchi, jambo litakalotafsiriwa kama kitendo cha kizalendo.

Aidha, Meneja Mwandamizi wa Mahusiano wa benki ya NMB, Dorah Monyo alisema utaratibu wa kuweka fedha kwenye benki za ndani utakuwa na faida kubwa kwa wananchi kwani mzunguko wa fedha unabaki ndani.

Pia alimuahidi Waziri mkuu kuwa NMB itakuwa benki ya kwanza kusaidia mashirika hayo kuwa na akaunti ndani ya benki na zenye uendeshaji wa gharama nafuu.

Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali, Dk. Lilian Badi alisema ni wakati kwa taasisi binafsi kuwekeza fedha zao kwa mabenki ya nyumbani ili kuchangia ukuaji wa uchumi.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (kulia) akijadiliana jambo na wafanyakazi wa Benki ya NMB alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Jukwaa la mwaka la Mashirika yasiyo ya Kiserikali lilolofanyika Jijini Dodoma. Benki ya NMB ni mmoja wa wadau wa jukwaa hilo.

Pia, aliiomba Serikali kuzipa nafasi taasisi zisizo za kiserikali ikiwemo kuwapa uhuru wa kufanya majukumu yao kwani kwa sasa wamebanwa hasa kipengele cha usajili wa miaka 10.

Alisema kifungu hicho kinawakosesha nafasi ya kujadiliana na wadau kuhusu miradi mikubwa.

1 Comment

  • Uzalendo peke yake hautoshi. NMB inapaswa washindane na mabenki mengine yaliyoruhusiwa nchini. Kama NMB inashindwa kushindana na wenzao basi serikali itaendelea tu kutoa wito kwa NGO
    Wakati huo huo serikali iache kulazimisha mishahara na pensheni zake zipitie NMB. Waacheni wateja wajichagulie benki wazipendazo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!