Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Matokeo ya darasa la Saba haya hapa
ElimuTangulizi

Matokeo ya darasa la Saba haya hapa

Wanafunzi wakishangilia baada ya kumaliza mtihani wa darasa la saba
Spread the love

BARAZA la Mitihani nchini (NECTA), limetangaza matokeo ya darasa la saba ambapo Mikoa ya Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kushika nafasi 10 za mwanzo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Angalia hapa matokeo yote ya darasa la saba 2019

Akitangaza matokeo hayo leo tarehe 15 Oktoba 2019, Dk. Charles Msonde, katibu mtendaji wa baraza hilo amesema, ufaulu umeongezeka kwa asililia 3.78.

Msonde amesema, asilimia 81 ya watahiniwa wamefauli mtihani huo huku wanafunzi 909, wakifutiwa matokeo yao kutokana na udanganyifu.

Amesema, pamoja na matokeo hayo, tatizo kubwa lipo katika somo la Kiingereza ambalo ufaulu wake umepungua huku akiagiza juhudi zaidi kufanyika.

Kwenye matokeo hayo, mikoa ya Kanda ya Ziwa imeonekana kufanya vizuri zaidi kulinganisha matokeo ya mwaka jana na miaka iliyopita.

Msonde ametaja shule 10 bora kuwa ni Graiyaki (Mara), Twibhoki (Mara), Kemebos (Kagera), Little Treasures (Shinyanga), Musabe (Mwanza), Tulele (Mwanza), Kwema Morden (Shinyanga), Peaceland (Mwanza), Mugini (Mwanza) na Rocken Hill (Shinyanga).

Katika ufaulishaji watoto wengi Msonde amesema, Mkoa wa Dar es Salaam umeshika nafasi ya kwanza ukifuatiwa na Arusha, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Mbeya, Simiyu, Njombe na Pwani.

Kwenye matokeo hayo, Msonde ametaja wanafunzi walioshika nafasi ya 10 za mwanzo kuwa ni Grace Imori Manga (Graiyaki), Mara; Francis Gwani (Paradise) Geita na wa tatu ni Loi Kitundu (Mbezi), Dar es Salaam.

Wengine ni Victor Godfrey, Azizi Yassin na Goldie Hhayuma wote wa Graiyaki, Mara; Daniel Daniel (Little), Shinyanga; Hilary Nassor (Peaceland), Mwanza; Mbelele Mbelele (Kwema Modern), Shinyanga na Nyanswi Richard wa Graiyaki (Mara).

6 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!