Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Marufuku kuingia mkataba bila kumshirikisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Habari za Siasa

Marufuku kuingia mkataba bila kumshirikisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepiga marufuku mamalaka yeyote ya Serikali kuingia mkataba bila kuishirikisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Amesema hatua hiyo inakuja baada ya kuwepo kwa mikataba inayoingiwa bila kuishirikisha ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali lakini mgogoro unapotokea mamlaka husika kwenda kuomba msaada kwa ofisi hiyo.

Samia ametoa agizo hilo leo Alhmisi Tarehe 29, Septemba, 2022, wakati akizungumza na Mawakili wa Serikali kwenye Mkutano wao Mkuu wa Chama ambacho kimeanzishwa rasmi na kuzinduliwa jijini Dodoma.

“Kuna mikataba watu wanajiingilia tu huko halafu  ikitokea shida huko wanakimbilia kwa AG tusaidie, mliingiaje mikataba AG hajui, na pengine aliyeingia alishastaafu hayapo na pengine hayupo duniani kwahiyo kupata chanzo inasumbua kwahiyo niombe sana na hii ni kwa Serikali nzima kwamba hakuna mkataba utakaoingiwa bila kushirikisha ofisi ya mwanasheria mkuu,” amesema Rais Samia.

https://youtu.be/fLMVAMHcx9s

Aidha Mkuu huyo wan chi amewataka mawakili wa Serikali kutekeleza majuku yao kwa weledi na uadilifu katika kushuhulikia mashaur ya uwekezaji ili kusaidia kukuza uchumi na pato la Taifa.

Amewataja mawakii hao kama jeshi la kulinda uchumi wa Taifa hasa katika kipindi hiki ambacho Seerikali imehamasisha uwekezaji ambao amesema utakuja na migogoro mbalimbali ya kiuwekezaji ambayo itahitaji utatuzi.

Amesema ili kukuza uchumi ni lazima migogoro hiyo itatuliwe kwa haki na pengine ishughulikiwe kabla ya kufikishwa mahakamani iwe imetatuliwa.

1 Comment

  • Hongera sana!
    Hakikisha hakuna vichwa kama vya Chenge na Muongo.
    Machimbo ya mashimo ya wazi kwenye madini tusiwape wawekezaji wa nje.
    Makampuni mengi ya wawekezaji yamesajiliwa kwenye nchi marafiki lakini ni ya uongo. Tuchunguze kazi walizofanya na si kwenda ubalozi na kuulizia.
    Nakupongeza…kaza kamba na endelea na uwazi.
    Hongera sana!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!