Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia ataka Sheria ya kulinda uwekezaji iangaliwe upya
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ataka Sheria ya kulinda uwekezaji iangaliwe upya

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonesha kutoridhika na masharti ya sheria ya kulinda uwekezaji inayoweka ulazima wa mzozo baina ya mwekezaji na Serikali kuamuliwa hapa nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa Serikali uliofanyika leo Alhamisi tarehe 29 Septemba 2022 jijini Dodoma, Rais Samia amesema Sheria hiyo hailetoi picha nzuri kwa wawekezaji na badala yake inawafukuza na kumtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwenda kuitizama.

Mkuu huyo wa nchi amesema anayo mifano ya wawekezaji wanne waliokuwa tayari kuwekeza fedha nyingi kwa sharti la kutaka mizozo itatuliwe na mtu wa tatu lakini Serikali imeshindwa kwasababu ya uwepo wa Sheria hiyo.

“Nchi yetu inaingia mikataba mikubwa tu na nafahamu sheria zetu zinataka tunapopata mzozo na mwekezaji aanze au atumie Sheria zetu za ndani. Lakini kama mtu anakuja na fedha yake kubwa inaiwekeza ndani ya nchi tunakwenda na uwekezaji ule, mzozo unapotokea tunamwambia mimi nitakuhukumu, umekuja na fedha zako umekuja kuwekeza kwangu lakini ukitokea mzozo mimi nitakuhukumu nadhani haileti sura nzuri sana kwa wawekezaji na wengine wanatukimbia kwasababu hiyo,” amesema Rais Samia.

“Nina mifano hai mkononi kuna miradi mikubwa mitatu minne hivi , wawekezaji wamekuja na fedha nyingi sana, tumefanya mazungumzo tumefika katikati mwekezaji anasema unapotokea mgogoro twende kwa mtu wa tatu, usije kwangu, nisihukumiwe na wewe, twende kwa mtu wa tatu, sisi tukasema hapana mimi nitakuhukumu mwenyewe sasa wewe umekula pesa yake, amekupa ajira, uwekezaji upo kwako ukitokea mzozo unasema mimi nitakuhukumu tuwe wa kweli kuna haki hapo? amehoji Rais Samia.

“Pamoja na kwamba tunasema kwenye Sheria ya kulinda uwekezaji tuitizame vizuri, kuna mashauri kweli tunaweza kuyafanya hapa ndani lakini kuna ambayo mwekezaji ukimpa kipengele anakimbia. Niombe Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ukaitazame hii nyie ndo wataalamu.”

1 Comment

  • Hongera kwa kuanzisha haya mazungumzo.
    Serikali za nchi zilizoendelea haziingii mikataba na makampuni binafsi ya nje. Bali wanawawezesha wazawa asilia halafu makampuni ya wazawa asilia yanaingia mikataba na makampuni ya nje.
    Pia watakiwe kuingia soko la hisa Dar baada ya miaka mitatu hata kama watajiuza kwa kampuni nyingine mpya.
    Nakutakia kazi njema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!