Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda: Mbowe mnufaika namba 1 wa maridhiano ya kisiasa
Habari za SiasaTangulizi

Makonda: Mbowe mnufaika namba 1 wa maridhiano ya kisiasa

Spread the love

Katibu wa NEC – Itikadi na Uenezi (CCM) Paul Makonda amesema Mwenyekiti wa Chadema, Freema Mbowe ni mnufaika mkubwa wa maridhiano ya kisiasa kati ya CCM na Chadema kwani ndio yamefanya kuwa huru baada ya kuachiwa bila masharti katika kesi mbalimbali huku kesi zote za kisiasa zikifutwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema Mbowe anafahamu katika mapendekezo 84 yaliyotolewa, mapendekezo 63 yote yamechukuliwa na yapo kwenye miswada ambayo hatua za kisheria zinaendelea ili kuwa sheria kamili.

“Pia  chama chake na vingine vikaruhusiwa kufanya mikutano ya hadhara bila kubughudhiwa tena kwa mlinzi mkali chini ya Jeshi la Polisi kuhakikisha dhamira ya Rais Samia inatimia si tu kwa vyama vya siasa bali kwa Watanzania wote.

Aidha, ameongeza kuwa kila alichosema Mbowe, Rais Samia aliridhia na wakati mwingine alikubali kukinzana na wana CCM wenzake ili kujenga mustakabali mpana wa Taifa moja lisilobaguana na vyama.

“Lakini matokeo yake jana Mbowe katangaza tena kuacha mchakato huu wenye dhamira njema na kukimbia mtaani kuhamasisha maandamano” amesema Makonda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!