CHAMA Cha ACT-Wazalendo kimeitaka Serikali kuwawekea mazingira mazuri wafanyabiashara ndogondogo maarufu ‘machinga’ yatakayowawezesha kufanyabiashara zao na si kuwakimbiza na kuwamwaga bidhaa zao. Anaripoti Faki Sosi, Arusha (endelea).
Akizungumza leo tarehe 14 Januari 2023 katika uzinduzi Mkutano Mkuu wa chama hicho wa mkoa wa Arusha ulioambatana na uchaguzi wa viongozi wa mkoa huo, Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bara, Dorothy Semu amesema kuwa kitendo cha wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga cha kunyanyaswa na askari wa jiji hakivumiliki.
“Hiki ni kilio cha nchi mzima sisi ACT -Wazalendo tunataka kujenga taifa litakalowaheshimu wafanya baishara wanawekewa mazingira mazuri biashara zao zitastawi, watafanya biashara kwa amani “
Amesema kuwa kisingizio cha kuwa wafanyabiashara wanachafua miji hakikubaliki.
“Tunasimama na wafanyabiashara tunaitaka Serikali ya Arusha kuhakikisha wanaweka mazingira bora kwa ajili ya wafanyabiashara.”
Leave a comment