WAZIRI mkuu Kassim Majaliwa ameeleza kuridhishwa na kasi ya ukusanyaji mapato uliopo katika halmashauri ya mji Tunduma wilayani Momba mkoani Songwe huku akimsisitiza mkurugenzi wa mji huo, Philimon Magesa kuendeleza kasi hiyo bila kujali figisu zilizopo. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea).
Majaliwa ametoa pongeza baada ya Mkurugenzi huyo kudaiwa kuminya mianya ya wizi wa fedha za halmashauri katika ukusanyaji mapato ambapo baadhi ya watendaji walizoea kula fedha mbichi wakiendesha ushawishi kwa baadhi ya madiwani ili kuendesha hujuma ili aonekane hafahi.
Waziri mkuu ambaye yupo kwenye ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani Songwe amewaeleza wananchi kupitia mkutano wake kuwa mkurugenzi huyo ameaminiwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na ndiyo maana yupo Tunduma na kasi ya ukusanyaji mapato imeonekana.
Alisema wakati anaingia kufanya kazi katika halmashauri hiyo alikuta makusanyo ya fedha za mapato ya ndani ni Sh bilioni tano lakini kwa muda wa mwaka mmoja wa uongozi wake mapato yameongezeka na kwamba katika mwaka huu wa fedha amefanikiwa kukusanya Sh bilioni nane kabla hata ya mwaka wa fedha haujaisha.
‘’Madiwani mlindeni mkurugenzi wenu, ametumia akili kubwa kuifanya halmashauri hii kupaa kimapato, sitegemei kuibuka migogoro, wakuu wa Idara ongereni sana, kwa kazi nzuri na ushirikiano mlio nao kwa madiwani.
“Kitendo cha kukusanya fedha kubwa kabla ya muda mnapaswa kupongezwa,nataka wakurugenzi wa halmashauri zingine ikiwemo Lindi jimboni kwangu waje kujifunza Tunduma’’alisema Waziri mkuu Majaliwa.
Naye Mbunge wa jimbo hilo,David Silinde alisema anafahamu uwezo wa mkurugenzi huyo toka alipokuwa halmashauri ya wilaya ya Nzega ambapo alifanikiwa kukusanya mapato maradufu.
Amesema ujio wake kwenye halmashauri ya mji Tunduma, kwake haukuwa na shaka na sasa wameona matunda katika vyanzo hivyo hivyo ameweza kuvuka lengo kabla hata mwaka wa fedha haujamalizika.
Aidha, Silinde ambaye ni Naibu waziri katika ofisi ya Rais (TAMISEMI ) anayeshughulikia elimu,amesema kutokana na makusanyo hayo wameweza kujenga miradi mbalimbali mikubwa zikiwemo shule za ghorofa na miradi ya afya kwa mapato ya ndani.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji Tunduma, Philimon Magesa ameishukuru Serikali kwa kumuamini na kwa jitihada za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amewapatia vinu na mitambo ya kuzalisha gesi kwa ajili ya matumizi ya hewa ya Oxjeni itakayotumika kusaidia wagonjwa wenye uhitaji.
Kama UMEPEWA PROJECT KITAMKWACHO HAYA TUTAONANA TENA YAWEE… TUTAONANA TENA.. TUTAONANA YAWE… TUTAONANA TENA… BIBI YAKO MPYA YAWEZEKANA ALIFIKA HUKU.. Je UNATAFUTA MWANAMKE NA HAUJAOA!? NUNUA PINDA HONEY… HUYU HAPA YUPO AVAILABLE..
https://www.picuki.com/media/2040637081931345491