Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba anusurika kifo akitoka kuhutubia mkutano wa hadhara
Habari za Siasa

Prof. Lipumba anusurika kifo akitoka kuhutubia mkutano wa hadhara

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba na wenzake watano, wamenusurika kifo baada ya kupata ajali maeneo ya Kilwa mkoani Lindi, akitokea Nanguruku alikokuwa anahutubia mkutano wa hadhara. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online, leo Alhamisi, tarehe 16 Februari 2023, Mkurugenzi wa Habari CUF, Mhandisi Mohamed Ngulangwa, amesema ajali hiyo ilitokea jana Jumatano, majira ya saa 1.00 usiku, baada ya gari alilopanda Prof. Lipumba kupinduka.

Mhandisi Ngulangwa amesema, Prof. Lipumba alikuwa njiani kuelekea Kilwa Kivinje, kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wa hadhara ulipangwa kufanyika leo.

Amesema wahanga wa ajali hiyo walipata majeraha madogo na kwamba walifikishwa hospitalini kwa ajili ya matibabu hivyo hali zao kiafya zinaendelea vizuri.

“Gari iliyopinduka haikuwa na tatizo, mwendo kasi haukuwa mkubwa lakini gari ilipinduka. Tunachoshukuru pamoja na kwamba gari iomeharibika vibaya lakini hakuna mtu aliyeumia sana ni majeraha madogo,” amesema Mhandisi Ngulangwa.

Alipoulizwa kama Prof. Lipumba ataweza kuhutubia mkutano wa hadhara wa leo, Mhandisi Ngulangwa amejibu akisema kwa sasa ni mapema mno kusema kama suala hilo litawezekana au lah, huku akieleza kwamba, kama itashindikana kuna uwezekano mkutano huo ukaahirishwa hadi kesho tarehe 17 Februari 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!