Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Mabondia wa Tanzania kunolewa Cuba
Michezo

Mabondia wa Tanzania kunolewa Cuba

Spread the love

 

TANZANIA kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na Serikali ya Cuba kupitia Taasisi ya INDER ya nchini humo zimekubaliana kushirikiana katika eneo la kuendeleza mchezo wa ngumi, ambapo mabondia kutoka nchini watapata fursa ya kuweka kambi Cuba.

Pia walimu wa ngumi na Mabondia kutoka Cuba watapata fursa ya kuja Tanzania kufundisha na kubadilishana ujuzi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Makubaliano hayo yamefikiwa juzi tarehe 2 Agosti 2023 wakati Naibu Waziri wa wizara hiyo, Hamis Mwinjuma alipofanya mazungumzo na Raul Fornes Valenciano ambaye ni Makamu wa Rais wa kwanza wa Taasisi hiyo ya Kitaifa ya Michezo, Elimu na Burudani ambacho ni chombo kinachohusika na ukuzaji wa michezo, elimu ya viungo na burudani nchini Cuba.

Taasisi hiyo tayari ina mashirikiano na baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Algeria ambapo hubadilishana uzoefu kwenye eneo la mchezo wa ngumi.

Naibu Waziri Mwinjuma yupo nchini Cuba kwa ajili ya kuhudhuria maonesho ya kimataifa ya michezo ya Havana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!