Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Nitafuta sheria hizi nikiingia Ikulu
Habari za Siasa

Lissu: Nitafuta sheria hizi nikiingia Ikulu

Spread the love

TUNDU Lissu, mbombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameahidi kufuta sheria zote kandamizi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Ametoa ahadi hiyo jana Jumatatu tarehe 31 Agosti 2020, akiwa kwenye kampeni za kusaka urais zilizofanyika katika viwanja vya Relini, jijini Arusha.

“Tanzania ya Tundu Lissu baada ya tarehe 28 Oktoba, tutafanya marekebisheo makubwa katika mfumo wa kisheria kuhusu kesi za jinai na nitafanya haraka kabisa,” alisema Lissu.

Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara alisema, endapo atachaguliwa kuwa Rais wa Tanzania, atarekebisha mfumo wa sheria kuhusu kesi za jinai, ili kuondoa sheria zinazonyima watuhumuwa dhamana, hasa wa utakatisha fedha na uhujumu uchumi.

“Kitu kikubwa ambacho kinasababisha mateso haya ya makesi ya uongo chanzo kikubwa ni kwamba, kuna masheria ya ukandamizaji ambayo yametengeza makosa yasiyokuwa na dhamana, ukipigwa utakatishaji fedha unaozea gerezani hakuna dhamana,” alisema Lissu.

“Tanzania ya Tundu Lissu itafuta sheria zote zinazonyima watu dhamana, Katiba yetu inasema, mahali kila mtu anahesabika kuwa hana hatia hadi hapo hatia yake itathibitishwa mahakamani, maana yake kama Katiba inasema huna hatia, hutakaa gerezani sababu umetuhumiwa tu.”

Lissu aliahidi kuifuta machozi nchi ya Tanzania pamoja na kurudisha umoja wa wananchi hasa wa jiji la Arusha.

“Arusha ya ujana wangu ilikuwa Arusha ya amani, ilikuwa Arusha ya upendo na watu kusaidiana, Arusha ya leo ya watu ambao wanateswa kwa miaka mitano, wamenyang’anywa pesa zao.”

“Arusha ya leo ni ya machozi damu na  vilio kwa sababu ya ukandamizaji wa miaka mitano, baada ya tarehe 28 Oktoba nitafuta machozi ya Arusha, nitafuta machozi ya Tanzania,” aliahidi Lissu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Tunastawisha ufisadi na kuchukia matunda yake

Spread the loveBUNGE la Jamhuri linaloendelea mjini Dodoma, kwa wiki nzima limetawaliwa...

error: Content is protected !!