Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Hakuna kuzaa kwa mpango
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Hakuna kuzaa kwa mpango

Rais John Magufuli, Mgombea wa Urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
Spread the love

DAKTARI John Magufuli, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema hakuna haja ya watu kuzaa kwa mpango kwa kuwa Serikali yake inatoa elimu bure. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Mgombea huyo wa CCM katika nafasi ya Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano wa tarehe 28 Oktoba 2020 ametoa kauli hiyo leo tarehe 1 Septemba 2020,  katika mkutano wake wa kampeni ulioanyika Ikungi mkoani Singida.

“Tunataka watoto wasome bure, ndio maana siku zote nilikuwa nasema zaeni  hakuna kuzaa kwa mpango, matiti ya kunyonyesha watoto tunayo, maziwa tunayo na wanaume wapo wakina mama wapo na shule wanasoma bure serikali ipo,” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewataka wakazi wa Ikungi na Watanzania kwa ujumla bila kujali tofauti za vyama vya siasa, kumpigia kura ili Serikali yake iendelee kutoa elimu bure.

“Asije akaja mwingine akageuza badala ya katoa elimu bure, watoto wakaanza kudaiwa, tutakuwa tunarudi nyuma.”

“Kwa nini turudi nyuma tulikotoka? Na ndio maana tunasema katika miaka mitano ijayo, tutatoa elimu bure ndio maana tunaomba ndugu zangu mturudishe,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli anaendelea na kampeni zake alizozizindua Jumamosi tarehe 29 Agosti 2020 jijini Dodoma, ambapo leo asubuhi alianzia Bahi mkoani Dodoma na kisha kuendelea Ikungi mkoani Singida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!