Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Sitanii, hili nitafanya Kinondoni
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Sitanii, hili nitafanya Kinondoni

Saed Kubenea, mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya ACT Wazalendo
Spread the love

SAED Kubenea, mgombea ubunge katika Jimbo la Kinondoni, jijini Dar es Salaam mesema miongoni mwa mambo ambayo atayasimamaia hadi kufanikiwa kwake ni suala la kutoa mikopo kwa vijana pamoja na mbinu za ‘kutumia pesa kuzalisha pesa.’ Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kubenea ametoa kauli hiyo leo Jumapili tarehe 27 Septemba 2020 kwenye Viwanja vya Buibui jijini humo wakati wa uzinduzi wa kampeni zake kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Akizungumza kwenye mkutano wake amesema, kipaumbele cha kwanza ni uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kutumia fedha za mfuko wa jimbo, ambazo atazitumia kutoa mikopo pamoja na kuwajengea uwezo wananchi kuzalisha pesa.

“Nataka kuboresha mfuko wa bunge na kutoa zaidi ya asilimia 80 ya fedha kwa ajili ya kuboresha masilahi ya wananchi wa Kinondoni, nitatoa mikopo na kuwapa elimu ya ujasiriamali wananchi,” amesema Kubenea.

Amesema, jambo la pili ni utatuzi wa changamoto ya mafuriko kwa kupanua Mto Msimbazi na Mto wa Ng’ombe, kwa kutafuta fedha za utekelezaji wa miradi hiyo kwa wafadhili.

“Nataka kutoa kero ya mafuriko na bahati nzuri, fedha zipo za kupanua Mto Msimbazi na kuubadilisha kuwa kivutio cha utalii, Benki ya Dunia ilitaka kutoa fedha lakini haijatoa sababu serikali inasusua tunataka kuchukua halamshauri ili suala hilo likawe historia,” amesema Kubenea.

Ahadi ya tatu aliyoitoa mbele wa wananchi na wanachama waliohudhuria mkutano wake ni ujenzi wa Shule ya Kidato cha Tano na Sita, ili kuondoa kero kwa wanafunzi kwenda kutafuta elimu katika majimbo jirani.

“Halmashauri ya Kinondoni haina shule ya Kidato cha Tano na Sita. Tunataka tujenge shule ili watoto wetu wasiende mbali kutafuta elimu,” amesema Kubenea.

Pia ameahidi utatuzi wa changamoto ya uchafu wa mazingira kwa kuifanya kuwa fursa ya kiuchumi kwa kuanzisha kiwamda cha uchakataji taka kuwa mbolea.

Kubenea amesema, ujenzi wa kiwanda hicho utasaidia kuzalisha ajira kwa wananchi na kufanya mazingira kuwa safi na salama.

“Nataka tugeuze taka kuwa ajira sababu ukitengeneza taka kuwa mbolea utaajiri watu. Nitaanzisha kiwamda cha taka,” ameahidi Kubenea aliyekuwa mbunge wa Ubunge kupitia Chadema kati ya 2015-2020.

Akijinadi katika mkutano huo, Kubenea amewaomba wananchi wa Kinondoni wamchague kwa kuwa anauzoefu na kazi za bunge lakini pia ni mwanasiasa muaminifu asiyenunulika.

“Ninalifahamu bunge vizuri na nafahamu kazi za mbunge, nimekuwa mbunge mniamini sinunuliki, sina bei naahidi kuwatumikia kwa uaminifu mkubwa. Sitababaishwa na kauli za rejareja wala kauli za uongo. Ukichagua mbunge ambaye anajua kazi za mbunge, anajua maana ya mbunge maendeleo katika maeneo yenu yatapatikana kwa haraka sana,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, amemua kugombea Ubunge Kinondoni ili asimamie maendeleo ya wananchi wa jimbo hilo.

“Ndugu zangu wa Kinondoni, mimi nataka kuwa mbunge wa Kinondoni ili nisimamie maendeleo na masilahi ya wananchi wa Kinondoni,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, “Kuna tofauti ya mbunge anayetokana na wananchi na anayetafuta ubunge kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na mbunge anayekwenda kutumikia chama chake na baishara zake, hiyo tofauti lazima muielewe.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!