Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sheikh Katimba: 28 Oktoba fursa wapinzani kupumua
Habari za Siasa

Sheikh Katimba: 28 Oktoba fursa wapinzani kupumua

Sheikh Rajab Katimba kutoka Taasisi ya na Jumuiya za Kiislamu Tanzania
Spread the love

SHEIKH Rajab Katimba kutoka Taasisi ya na Jumuiya za Kiislamu Tanzania amesema, Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020 utumike kama fursa ya upinzani nchini humo kupumua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Sheikh Katimba amesema hayo leo Jumapili tarehe 27 Septemba 2020 katika uzinduzi wa kampeni za Mgombea Ubunge wa  Kinondoni kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Saed Kubenea uliofanyika Viwanja vya Buibui jijini Dar es Salaam.

Amesema, vitendo vya vyama vya upinzani kuhujumiwa katika michakato ya uchaguzi vinapaswa kukomeshwa kwa kuiondoa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani kupitia uchaguzi huo.

https://youtu.be/YHmWaSZmvI8

“Wapinzani ndio wenye kushughulikiwa,  kuenguliwa wao. Tumeshuhudia mwaka jana wapinzani wamebanwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, hii sio fursa ya kuichezea, inatakiwa kila mtu kuitumia kura yake kuhakikisha ufisadi tunauondoa sababu Mungu hapendi ufisadi,” amesema  Sheikh Katimba.

Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba 2019, CCM ilishinda uchaguzi huo kwa zaidi ya asilimia 95 baada ya baadhi ya vyama vya upinzani kususia uchaguzi huo kutokana na wagombea wake wengi kuenguliwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo kutokidhi masharti ya ujazaji fomu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!