SHEIKH Rajab Katimba kutoka Taasisi ya na Jumuiya za Kiislamu Tanzania amesema, Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020 utumike kama fursa ya upinzani nchini humo kupumua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Sheikh Katimba amesema hayo leo Jumapili tarehe 27 Septemba 2020 katika uzinduzi wa kampeni za Mgombea Ubunge wa Kinondoni kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Saed Kubenea uliofanyika Viwanja vya Buibui jijini Dar es Salaam.
Amesema, vitendo vya vyama vya upinzani kuhujumiwa katika michakato ya uchaguzi vinapaswa kukomeshwa kwa kuiondoa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani kupitia uchaguzi huo.
https://youtu.be/YHmWaSZmvI8
“Wapinzani ndio wenye kushughulikiwa, kuenguliwa wao. Tumeshuhudia mwaka jana wapinzani wamebanwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, hii sio fursa ya kuichezea, inatakiwa kila mtu kuitumia kura yake kuhakikisha ufisadi tunauondoa sababu Mungu hapendi ufisadi,” amesema Sheikh Katimba.
Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba 2019, CCM ilishinda uchaguzi huo kwa zaidi ya asilimia 95 baada ya baadhi ya vyama vya upinzani kususia uchaguzi huo kutokana na wagombea wake wengi kuenguliwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo kutokidhi masharti ya ujazaji fomu.
Leave a comment