Saturday , 10 June 2023
Home Kitengo Michezo Kocha wa Simba afichua siri ya ushindi dhidi ya Yanga
MichezoTangulizi

Kocha wa Simba afichua siri ya ushindi dhidi ya Yanga

Spread the love

BAADA ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga, kocha mkuu wa Simba, Patrick Aussems, amedai kuwa klabu yake ilistahili kushinda mchezo huo wa watani wa jadi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo uliohudhuriwa na maelfu ya wapenda soko jijini Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, Aussems amesema, “tulistahili kushinda. Tulitengeneza nafasi nyingi sana. Tunamshukuru Mungu tumeshinda.”

Amesema, licha ya kucheza mechi ngumu hivi karibuni, wachezaji wake walijitahidi kucheza vizuri na kuwapongeza kwa kile walichokifanya.

“Leo niwe mkweli baada ya dakika ya 60 hadi 65 tulivyogongesha mwamba na kutengeneza nafasi nyingi nilishaanza kufikili kama yale yale yaliotokea katika mchezo uliopita. Lakini nashukuru kuwa baadae tulifanikiwa kupata bao,” alieleza.

Aussems amesema, “nafikili tulistahili kushinda na nawapongeza wachezaji wangu kwa kuwa walicheza mechi ngumu siku nne zilizopita na kwamba nina furaha ya ushindi na najivunia kuwa nao.”

Goli pekee la Simba katika mchezo huo lilifungwa na mshambuliaji wao Meddy Kagere, katika dakika 71 ya mchezo kwa njia ya kichwa.

Jikumbushe sehemu ya mchezo huo kwa kufuatilia  video kamili hapa chini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!