Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha wa Simba afichua siri ya ushindi dhidi ya Yanga
MichezoTangulizi

Kocha wa Simba afichua siri ya ushindi dhidi ya Yanga

Spread the love

BAADA ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga, kocha mkuu wa Simba, Patrick Aussems, amedai kuwa klabu yake ilistahili kushinda mchezo huo wa watani wa jadi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo uliohudhuriwa na maelfu ya wapenda soko jijini Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, Aussems amesema, “tulistahili kushinda. Tulitengeneza nafasi nyingi sana. Tunamshukuru Mungu tumeshinda.”

Amesema, licha ya kucheza mechi ngumu hivi karibuni, wachezaji wake walijitahidi kucheza vizuri na kuwapongeza kwa kile walichokifanya.

“Leo niwe mkweli baada ya dakika ya 60 hadi 65 tulivyogongesha mwamba na kutengeneza nafasi nyingi nilishaanza kufikili kama yale yale yaliotokea katika mchezo uliopita. Lakini nashukuru kuwa baadae tulifanikiwa kupata bao,” alieleza.

Aussems amesema, “nafikili tulistahili kushinda na nawapongeza wachezaji wangu kwa kuwa walicheza mechi ngumu siku nne zilizopita na kwamba nina furaha ya ushindi na najivunia kuwa nao.”

Goli pekee la Simba katika mchezo huo lilifungwa na mshambuliaji wao Meddy Kagere, katika dakika 71 ya mchezo kwa njia ya kichwa.

Jikumbushe sehemu ya mchezo huo kwa kufuatilia  video kamili hapa chini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!