RIPOTI ya waandishi wa Habari wasiokuwa na mipaka duniani wanaosimamia tovuti ya ‘Just Earth News’ iliyotolewa mwezi Mei mwaka huu inaiweka China kuwa kwenye nafasi pili kwenye nchi zisizo kuwa na uhuru wa habari duniani ikizidiwa na Korea Kaskazini, Imeripotiwa na Business Standard …(endelea).
Ripoti hiyo kuwa waandishi wa habari na hata raia hawako salama ambapo wengine huchunguzwa na Chama tawala cha Kikomunisti cha China (CCP).
Tarehe 3 Mei inatambulika kimataifa kama Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ukumbusho ulioanzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 1993.
Azimio la Ulimwengu la Haki za Kibinadamu, lililoidhinishwa na UN, linakubali uhuru wa kujieleza kuwa haki ya msingi ambayo inaunda msingi wa kufurahia haki nyingine za binadamu.
Kuripoti ukweli ni gharama ndani ya China. Wakosoaji kama Fang Bin, Zhang Zhan, na Li Wenliang, ambao walifichua habari muhimu kuhusu janga la COVID katika hatua zake za awali, wanaendelea kuteswa wakiwa kizuizini na Serikali ya China.
Fang Bin, ambaye aliandika ukweli wa COVID-19, aliachiliwa kutoka gerezani Aprili 30 mwaka huu lakini anajikuta hawezi kurejea nyumbani kutokana na vitisho vilivyopokelewa na familia yake huko Wuhan. Bado Mamlaka zinamfuatilia Mwenendo wake.
Fung alifungwa kimyakimya hukumu ya kutumikia miaka mitatu jela tangu mwaka 2020.
Leave a comment