Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kisa machinga kuuza senene ndani ya ndege, waziri awatimua wafanyakazi
Kimataifa

Kisa machinga kuuza senene ndani ya ndege, waziri awatimua wafanyakazi

Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi na Usafirishaji nchini Uganda, Jenerali Edward Wamala ameagiza kusimamishwa kazi wafanyakazi wa Shirika la Ndege la Uganda baada ya video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii ikimuonesha mmoja wa wamachinga nchini humo akiwauzia senene abiria ndani ya ndege ya shirika hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Video hiyo iliyoanza kusambaa jana tarehe 27 Novemba, 2021 imemuonesha mwanaume huyo ambaye bado hajafahamika jina akiwauzia kitowea hicho abiria.

Mmachinga huyo ambaye pia haijafahamika nani alimrekodi video hiyo, alikuwa amewahifadhi senene hao kwenye mfuko wa bluu na kuwauzia abiria waliokuwa wamekaa kwenye daraja la kawaida.

“Ni Shilinga za Uganda 10,000 (sawa na Shilingi za kitanzani 6,400 )” alisikika mwanaume huyo akiwatangazia abiria waliokuwa wamekaa katika ndege hiyo aina ya Airbus A330.

Waziri wa Ujenzi na Usafirishaji nchini Uganda, Jenerali Edward Wamala

Baadhi ya watu waliokaribu na Waziri huyo wameuleza mtandao wa Chimpreport kwamba, kiongozi huyo amekasirika kutokana na tukio hilo ambalo amesema ni la kutia aibu.

Hata hivyo, haijaelezwa ni wafanyakazi wangapi wamesimamishwa kazi, lakini tukio hilo limeibua mjadala mkubwa nchini humo.

Senene ni kitoweo pendwa katika ukanda wa Kagera na maeneo yanayozunguka mkoa huo uliojirani na nchi ya Uganda

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!