RAIS wa zamani wa Marekani, Donald Trump ameshtakiwa mara ya tatu ndani ya miezi minne iliyopita, sasa anatuhumiwa kula njama ya kutaka kubadilisha matokeo ya uchaguzi. Anaripoti Maryam Mudhihir, MUM … (endelea).
Mashtaka hayo yanadai kwamba alikula njama na watu wengine sita ambao majina yao haya kutajwa, kwa kutaka kubadili matokeo ya uchaguzi. Trump ameamriwa kufika katika mahakama ya serikali kuu alhamisi.
Kesi hiyo inatarajiwa kusikilizwa na Jaji wa Mahakama ya wilaya nchini Marekani Tanya Chutkan, aliyeteuliwa na rais wa zamani Barrack Obama.
Smith amesema anataka kesi hiyo katika taarifa, timu ya kampeni ya Trump imesema Trump amekuwa akifuata sheria kila mara na kuyataja mashtaka hayo kama ‘unyanyasaji’ wa kisiasa ule wa enzi za Ujerumani.
Trump amemsuta mwanasheria huyo maalum, akimuita kuwa aliyechanganyikiwa ma kumtuhumu kwa kile alichokiita shtaka bandia ili kuingilia uchaguzi wa rais.
Ameandika kwenye mtandao wake wa Truth social kuwa kwanini hawakuyafanya hayo miaka miwili na nusu iliyopita? kwanini walisubiri muda huu.
Leave a comment