Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Biashara Kampuni 5,000 zashiriki sabasaba
Biashara

Kampuni 5,000 zashiriki sabasaba

Spread the love

 

KAMPUNI 5666 za ndani na nje ya nchi zimeshiriki kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam DITF) maarufu kama Sabasaba yanayofanyika katika Viwanja vya Julius Nyerere jijini hapa. Anaripoti Selemani Msuya, Dar es Salaam … (endelea). 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dk Ashanti Kijaji wakati alipotrembelea maonesho hayo jana ambapo aliweka bayana kuwa idadi hiyo ya washiriki inaonesha namna gani Tanzania ni nchi nzuri kwa uwekezaji na biashara.

“Maonesho haya ya 47 yamekuwa ya mfano wa kuigwa tofauti na miaka mingine iliyopita kwani sasa hivi kampuni nyingi kutoka nje na ndani ya nchi yameshiriki niwaombe wananchi kuja kutembelea Sabasaba waone mambo mazuri,” alisema.

Dk Kijaji alisema zaidi ya kampuni 3,000 za Tanzania na 2,666 za nje ya nchi zimeshiriki maonyesho hayo hali inayosababisha kukuza ushirikiano wa kibiashara miongoni mwa nchi zilizoshiriki.

Aidha Dk Kijaji alisema kuwa kukutana kwa kampuni hizo na kushiriki kwa wingi zitasaidia kampuni za Tanzania kupata uzoefu kutoka katika kampuni hizo jambo litakalosaidia kuendeleza kampuni zao kisasa na kuongeza uzalishaji.

Alisema licha ya kampuni za ndani kupata ujuzi pia maonesho hayo yanafungua fursa kwa wawekezaji kuja nchini kuwekeza katika sekta mbalimbali.

“Naamini Maonesho haya ya 47 yataleta tija kwa kuwakaribisha wawekezaji wengine kuja nchini kuwekeza,”alisema Dk. Kijaji.

Alisema kampuni zàidi ya 150 kutoka nchini China kwa kutumia usafiri wa Shirika la Ndege la Tanzania kwaajili ya kuja kutembelea maonyesho haya.

“Hilo ndilo Rais wetu Samia Suluhu Hassan alisema anataka kufungua nchi na kuufungamanisha uchumini na shughuli zetu tunazofanya na ndio hili linaloendelea kutokea,” aliongeza Dk Kijaji.

Dk Kijaji alisema kutakuwa na makongamano mengi ya biashara ambayo yatatoa elimu na fursa za kibiashara wakati wa maonyesho na baada ya maonyesho ambapo kutakuwa na siku ya Irani, China na India kwa biashara ambapo siku hizo zitatangazwa fursa zinazopatikana kwenye nchi hizo, huku viongozi wakuu wa nchi hizo wakishiriki kwenye makongamano hayo.

Aidha, Waziri Kijaji aliwataka wafanyabiashara wa kitanzania kuendelee kuboresha na kubuni bidhaa nzuri kwa sababu wateja wapo na wanazipenda.

Naye Katibu Mkuu wa Chama Cha RPF Inkotanyi wa nchini Rwanda Komredi Wellars Gasamagera, alisema katika maonesho hayo kuna wafanyabiashara kutoka nchini Rwanda ambao wamefika kuonesha ubunifu wao mbalimbali.

“Tunashirikiana na nchi ya Tanzania katika mambo mengi ikiwemo namna ya kubadilishana ujuzi wa Biashara ili kukuza umoja na ushirikiano wa nchi zetu,” alisema Gasamagera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

Biashara

Cheza kwa kuanzia Sh 400 kushinda mgao wa Expanse Tournament kasino 

Spread the love  UKISIKIA bosi kacheka ujue Maokoto yanafuatia, Kupitia promosheni pendwa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Biashara

Mchezo wa maokoto Cobra Queen unapatikana Meridianbet

Spread the love Meridianbet Kasino Mtandaoni utapata fursa ya kufurahiamchezo uliochochewa na...

error: Content is protected !!