Bunge la Tanzania limesema, vikao vya kawaida vya Kamati za Kudumu za Bunge vitaanza kufanyika Jumatatu tarehe 14 hadi 25 Agosti 2023 Jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa 12 wa Bunge utakaonza tarehe 29 Agosti 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)
Taarifa kwa umma iliyotolewa na Ofisi ya Bunge leo Jumapili na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa imesema Kamati tano zitatangulia kuanza vikao.
Imesema nne kati ya hizo zitaanza vikao tarehe 7 Agosti 2023 na Kamati moja ya Bajeti itaanza tarehe 10 Agosti 2023.
Imefafanua kuwa shughuli za kamati katika kipindi hicho zitakuwa ni: -Uchambuzi wa Miswada miwili ya Sheria utakaofanywa na Kamati mbili: Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria na Kamati ya Bajeti;
Pili ni uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa wakati wa Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge na tatu ni chambuzi wa Taarifa za Hesabu zilizokaguliwa na CAG kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2022
Nne ni uchambuzi wa Taarifa za Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa lengo la kuliwezesha Bunge kufuatilia ufanisi na tija kwa Mitaji ya Serikali kwenye mashirika mbalimbali na taasisi; na mwisho ni uchambuzi wa Taarifa za Utendaji za Wizara kwa lengo la kuliwezesha Bunge kutekeleza jukumu la kuisimamia na kuishauri Serikali.
Leave a comment