Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Joe Biden amchefua Balozi Haiti, ajiuzulu
Kimataifa

Joe Biden amchefua Balozi Haiti, ajiuzulu

Balozi Daniel Foote
Spread the love

 

RAIS wa Marekani, Joe Biden amedaiwa kumchefua Mwakilishi wake maalumu nchini Haiti, Balozi Daniel Foote baada ya kukataa mapendekezo yake kuhusu njia bora ya kushughulikia suala la wahamiaji kutoka Haiti wanaokimbilia Marekani. Anaripoti Helena Mkonyi –TUDARCo … (endelea).

Siku chache baada ya Idara inayoshughulikia mambo ya nje ya Marekani, kukataa mapendekezo yake, jana tarehe 23 Septemba, 2021 Balozi huyo amemuandikia Katibu Mkuu wa Serikali wa Marekani Antony Blinken barua ya kujiuzulu wadhifa wake.

Balozi Foote amevieleza vyombo vya habari kuwa amejiuzulu kwa sababu wahamiaji zaidi ya 3000 wanaokimbilia Marekani wamerejeshwa Haiti bila kujali utu.

Joe Biden, Rais wa Marekani

Balozi huyo ambaye aliteuliwa kushika wadhifa huo Julai mwaka huu amesema licha ya kwamba Haiti ni nchi inayokabiliwa na majanga kama vile vimbunga, matetemeko ya ardhi huku hali ya kisiasa ikizidi kudorora baada ya Rais Jovenel Moise kuuawa, bado Marekani haionekana kuwajaliwa wahamiaji hao.

Aidha, kufuatia uamuzi huo Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imemkosoa Foote kwa kujiuzulu kwake katika kipindi kigumu ambacho Haiti inapitia.

Msemaji wa Idara ya Mambo ya nje ya Marekani, Ned Price  amekanusha madai ya wizara hiyo kutupa mbali mapendekezo ya balozi huyo lakini akaongeza kuwa Foote ameshindwa kuwa mvumilivu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!